RAIS MWINYI:SERIKALI ITAJENGA BARABARA NYINGI PEMBA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Barabara za Kilomita 10 za Micheweni - Kiuyu-Maziwa Ng'ombe na Barabara ya  Michweni -Shumba Mjini hadi Bandarini  Wilaya ya Micheweni , Mkoa wa Kaskazini Pemba.

.........................................

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewahakikishia Wananchi wa Pemba kuwa Barabara nyingi Kisiwani humo zitajengwa  kwa Kiwango cha Lami.

Rais Dk Mwinyi ameyasema hayo alipozindua  Barabara za Kilomita 10 za Micheweni - Kiuyu-Maziwa Ng'ombe na Barabara ya  Michweni -Shumba Mjini hadi Bandarini  Wilaya ya Micheweni , Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Aidha  amefahamisha kuwa Serikali ina Programu Maalum ya Kuziwekea Taa Barabara zote zilizojengwa kwa Kiwango cha Lami  nchi nzima.

Rais Dk.Mwinyi  amewahimiza Wananchi  kuacha kujenga  katika  Hifadhi za Barabara kwani zimetengwa maalum kwa ajili ya kuendeleza Miundombinu mengine.

Halikadhalika Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa  kumekuwa na  tabia ya watu kujenga Pembezoni mwa Barabara kwa kutegemea kulipwa Fidia na Serikali jambo ambalo sio sahihi.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amezitaka Halmashauri Kusimamia suala hilo  na kudhibiti Utoaji wa  vibali  holela vya Ujenzi Pembezoni mwa Barabara.

Akiwasilisha Taarifa ya Kitaalamu ya Ujenzi wa Barabara Katibu Mkuu  wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Dk, Habiba Hassan amesema Ujenzi wa Barabara hizo zenye Urefu wa  Kilomita 10 ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2025 ,Dira ya Maendeleo ya Zanzibar, Mpango Mkuu wa Maendeleo wa Taifa na Mpango Mkuu wa Usafiri  ambapo  Barabara zenye Urefu wa  Kilomita 140.9 zimejengwa  Unguja na  Kilomita 134.9 zimejengwa Pemba.

Hafla ya uzinduzi wa barabara hizo ikifanyika.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi (kulia ) akivuta pazia kuashiria uzinduzi wa Barabara hizo.
 

Post a Comment

Previous Post Next Post