MBUNGE WA MBEYA MJINI, DKT. TULIA ACKSON AWATAKA WANA CCM KUENDELEA KUWA WAMOJA Inbox

        Mbunge  wa Mbeya Mjini na Spika wa Bunge, ambaye pia ni  Rais                   wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU)Dkt. Tulia Ackson (kushoto) akiwa na     viongozi wa CCM Kata ya Nonde wakati alipofanya ziara Machi 2, 2025.

                                           ..............................................

                                             Na Zuhura Jafari, Mbeya

MBUNGE wa Mbeya Mjini na Spika wa Bunge, ambaye pia ni  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU)Dkt. Tulia Ackson amewataka Wana CCM Mkoa wa Mbeya kuendelea kuwa wamoja na kukijenga chama hicho.

Dkt. Ackson ameyasema hayo Machi 2, 2025 wakati alipokuwa akizungumza na wana CCM wa Kata ya Nonde jijini humo alipofanya ziara ya siku moja ya kuwatembelea kwa lengo za kujua kero walizonazo ili kuzitafutia ufumbuzi.

“Nawaombeni tuendelee kupendana na kushikimana hasa katika kipindi hiki tunachoelekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu,” alisema Dkt. Tulia.

Aliwaomba wana CCM hao wakati wa uchaguzi mkuu utakapo wadia wajitokeze kwa wingi kupiga kura na kuhakikisha wanampa kura nyingi Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha Dkt. Tulia aliwataka wana chama hao kuacha kuanzisha makundi ambayo yataweza kuwagawa wanachama jambo ambalo sio zuri kwani malengo yao ni kuhakikisha wagombea wote wa CCM wanapata ushindi mnono kuanzia, diwani, mbunge na Rais.

Mbunge  wa Mbeya Mjini na Spika wa Bunge, ambaye pia ni  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU)Dkt. Tulia Ackson akiwa katika picha ya pamoja na Wana CCM wa Kata ya Nonde.                                                          Picha ya pamoja.

Post a Comment

Previous Post Next Post